Numbers 26:28-33

28 aWazao wa Yusufu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:

29 bWazao wa Manase: kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi);
kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.

30 cHawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi:
kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri;
kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;

31 kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli;
kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;

32 kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida;
kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.

33 d(Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)

Copyright information for SwhKC